MCHAKATO WA BBI

Hakuna mtu atalazimisha Wakenya kupigia kura BBI- Kalonzo Musyoka

Kalonzo iwasihi Wakenya kutopinga BBI bila sababu.

Muhtasari

•"Hakuna mtu atakuja amebeba panga ama bakora akuambie lazima hiki kwa namna yoyote. Ni mambo ya kujadiliana na mafikra. Tuwe na mashindano ya mawazo kwani hati hii ni hati  ya mageuzi. Wacha tusiwe nchi pekee duniani ambayo  haina mageuzi. Wazo nzuri hutengeneza nafasi kwa wazo nzuri zaidi" Kalonzo alisema.

Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka
Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka
Image: MERCY MUMO

Kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka amewahimiza Wakenya kukumbatia mchakato wa BBI.

Akihutubia waumini katika kanisa ya Katoliki ya Kisooni, Kalonzo aliwaomba Wakenya kupitisha BBI kwani akisema kuwa italeta mageuzi nchini.

Hata hivyo, amewahakikishia wananchi kuwa hakuna yeyote atawalazimisha kupigia kura mchakato huo.

"Hakuna mtu atakuja amebeba panga ama bakora akuambie lazima hiki kwa namna yoyote. Ni mambo ya kujadiliana na mafikra. Tuwe na mashindano ya mawazo kwani hati hii ni hati  ya mageuzi. Wacha tusiwe nchi pekee duniani ambayo  haina mageuzi. Wazo nzuri hutengeneza nafasi kwa wazo nzuri zaidi" Kalonzo alisema.

Mwanasiasa huyo ambaye alikuwa mgombea mwenza wa kinara wa ODM, Raila Odinga kwenye uchaguzi mkuu wa 2017 aliwasihi Wakenya kutopinga BBI bila sababu.

Alisema kuwa mchakato huo ni wa Wakenya wote ila sio wa rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.

"Kuna watu ambao wanapinga jambo bila sababu yoyote. Mahakama ya kukata rufaa ikituruhusu  tutarudi kueleza wananchi maana na athari ya BBI. Hii ni hoja ya kutengeneza katiba. Hii kitu ni zaidi ya Uhuru Kenyatta na Raila Odinga, ni ya Wakenya wenyewe. Ni sharti tufikirie zaidi" Kalonzo alisema.