•Benson Njiru (22) na Emmanuel Mutura (19) ambao walikuwa wanafunzi katika chuo kikuu cha Kabarak na chuo cha mafunzo ya kiteknolojia cha Don Bosco mtawalia wanadaiwa kutoweka baada ya kukamatwa na polisi kutoka kituo cha polisi cha Manyatta mnamo Julai 1.
•Juhudi za kuwatafuta zilinoga kwa kipindi cha siku tatu zilizofuata hadi miili yao ikapatikana katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Embu Level 5 mnamo Jumanne wiki iliyopita.
•Wanamitandao waliojawa na ghadhabu kufuatia kukithiri kwa ripoti za matendo ya kikatili miongoni mwa maafisa wa usalama wameungana na familia ya marehemu kwenye vita ya kutafuta haki.
Maelfu ya Wakenya mitandaoni wamejumuika kudai haki kutendeka kufuatia kifo cha ndugu wawili kutoka maeneo ya Kianjokoma, Embu.
Benson Njiru (22) na Emmanuel Mutura (19) ambao walikuwa wanafunzi katika chuo kikuu cha Kabarak na chuo cha mafunzo ya kiteknolojia cha Don Bosco mtawalia wanadaiwa kutoweka baada ya kukamatwa na polisi kutoka kituo cha polisi cha Manyatta mnamo Julai 1.
Baada ya kukamatwa kwao haikujulikana walikokuwa na familia ikaanza juhudi za kuwatafuta.
Juhudi za kuwatafuta zilinoga kwa kipindi cha siku tatu zilizofuata hadi miili yao ikapatikana katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Embu Level 5 mnamo Jumanne wiki iliyopita.
Familia, marafiki na majirani wa ndugu hao wawili wameendelea kunyooshea maafisa wa polisi kidole cha lawama kufuatia kifo chao.
Wanamitandao waliojawa na ghadhabu kufuatia kukithiri kwa ripoti za matendo ya kikatili miongoni mwa maafisa wa usalama wameungana na familia ya marehemu kwenye vita ya kutafuta haki.
Chini ya alama ya reli #JusticeForKianjokomaBrothers kwenye mtandao wa Twitter, Wakenya wameendelea kushinikiza maafisa wa DCI kufanya upelelezi kuhusiana na tukio hilo kwa dharura na hatua kali kuchukuliwa dhidi ya wahusika.
Wanamitandao wengi wamelalamikia kulegea kwa wapelelezi katika uchunguzi wa tukio hilo na wameendelea kudai uchunguzi ukamilike haraka. Baadhi ya wanamiandao wametumia talanta na sanaa zao kudai haki ya ndugu hao ipatikane.
Hizi hapa baadhi ya jumbe za Wakenya;
We demand justice!!!#JusticeForKianjokomaBrothers pic.twitter.com/cqxtX3hoiL
— Erik Njiru (@TonyErik7) August 7, 2021
Heartbreaking as a mother to see the lives of these young men cut short through #PoliceBrutality. At what point do we say enough is enough? #JusticeForKianjokomaBrothers #Justice4Nyamai #blacklivesmatter pic.twitter.com/dw0uclA55u
— Dr. Roselyn Akombe (@DrRoselynAkombe) August 6, 2021
On Sunday, brothers Benson & Emmanuel Ndwiga were killed while in police custody.
— KHRC (@thekhrc) August 6, 2021
An autopsy report has revealed the two died from injuries due to a blunt object.
Police continue to kill too many innocent Kenyans without accountability.
We demand #JusticeForKianjokomaBrothers pic.twitter.com/1vhTUKVmLL
“If you are silent about your pain, they’ll kill you and say you enjoyed it.”- Zora Neale Hurston
— Boniface Mwangi (@bonifacemwangi) August 6, 2021
#JusticeForKianjokomaBrothers @IG_NPS @FredMatiangi pic.twitter.com/wYPFk4u3qY
These two brothers were brutally murdered by @PoliceKE in Embu. We demand Justice. Tag @DCI_Kenya on every post they make, force them to take action! #JusticeForKianjokomaBrothers pic.twitter.com/OCKuxelSGj
— Sir-Rap-A-Lot (@Osama_otero) August 9, 2021
If you are Kenyan, you are Emmanuel and Benson!
— #JusticeForKianjokomaBrothers (@ItsTrevorKe) August 7, 2021
Nothing special or specific!
Their injustice is injustice to us all!
It is hard to forget!#JusticeForKianjokomaBrothers pic.twitter.com/7Wr7rdCipk
Mnamo Ijumaa wiki iliyopita naibu inspekta Jenerali wa polisi Edward Mbugua aliagiza kuhamishwa kwa OCS wa kituo cha polisi cha Manyatta Abdullahi Yaya na OCPD wa Embu Kaskazini Emily Ngaruiya huku uchunguzi zaidi ukiendelea.
Wakuu katika idara ya polisi wakiongozwa na Mbugua walikutana na wakazi wa Embu ambao walikuwa katika siku ya tatu ya maandamano wakilalamikia mauaji ya ndugu hao wawili.