logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nina wasiwasi kuhusu mahakama ya Kenya'Seneta Ledama Olekina adai

Kulingana naye aliyekuwa Jaji Mkuu wa zamani Mutunga alisema kuwa wakati wake simu yao haikuweza kuita

image

Habari26 September 2022 - 18:01

Muhtasari


  • Mnamo Agosti 15 mahakama kuu ilimtangaza William Ruto kuwa rais wa tano wa jamuhuri ya Kenya

Seneta wa Narok H.E Ledama Olekina amedokeza kupitia ukurasa wake rasmi wa twitter akidai kuwa ana wasiwasi mkubwa kuhusu mahakama ya Kenya.

Kulingana naye aliyekuwa Jaji Mkuu wa zamani Mutunga alisema kuwa wakati wake simu yao haikuweza kuita hivi karibuni.

"Nina wasiwasi kuhusu Mahakama ya Kenya! Hivi karibuni simu Nyekundu ambayo Mutunga alisema haikuwahi kuita inaweza kuanza kuita". Seneta Ledama Olekina alisema.

Baadhi ya viongozi wa Muungano wa Muungano wa Azimio One Kenya Alliance wameendelea kulalamikia mahakama ya Kenya baada ya Azimio kushindwa katika ombi la urais katika mahakama kuu.

Mnamo Agosti 15 mahakama kuu ilimtangaza William Ruto kuwa rais wa tano wa jamuhuri ya Kenya.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved