logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilipata ameoa baada ya kutoka jela-Mwanamke asimulia

ndugu yake alinitembelea na kujaribu kunibaka jambo ambalo nilichukua kisu na kumdunga ilhali hakufa

image

Habari15 November 2022 - 16:05

Muhtasari


  • Nikiwa kwenye ziara yangu nilipatana na mwanamke, ambaye ana hadithi ya ajabu kuhusu maisha yake
  • Monicah ambaye alifungwa kwa miaka kadhaa, kwa kosa ambalo hakutarajia kwamba angepatana na mkono wa sheria, alisimulia jinsi mumewe alimsaliti
Mwanamke mwenye huzuni

Katika maisha ya kila mwanadamu kuna baadhi ya changamoto ambazo wanapitia licha ya kuamka kila siku na kusukuma gurudumu la maisha.

Kwa hakika kila mmoja ana hadithi ya kusimulia kuhusu maisha yao, kwa kile wamepitia na kuona.

Nikiwa kwenye ziara yangu nilipatana na mwanamke, ambaye ana hadithi ya ajabu kuhusu maisha yake.

Monicah ambaye alifungwa kwa miaka kadhaa, kwa kosa ambalo hakutarajia kwamba angepatana na mkono wa sheria, alisimulia jinsi mumewe alimsaliti.

"Mume wangu alikuwa ameniacha nyumbani pekeyangu wakati huo sikuwa nimemaliza miaka 5 katika ndoa wacha niseme nilikuwa mwanamke wa umri wa 29, ndugu yake alinitembelea na kujaribu kunibaka jambo ambalo nilichukua kisu na kumdunga ilhali hakufa

Baada ya tukio ndugu yake alisema kwamba nilikuwa nataka kumuua, na wala hakufanya jambo lolote na kwamba nimepagawa, bila ya kujua hivyo ndivyo nilifungwa jela kwa makosa ya kujaribu kuua

Kwa mwaka mmoja na nusu mume wangu alinitembelea na kunitia moyo, baada ya hapo sikuweza kumuona tena wala kusikia jina lake, baada ya kumaliza kifungo changu nilipata amemuoa mwanamke mwingine, na walahakujali nilichokuwa napitia nikiwa jela

Hakuonyesha kitendo cha kuniomba msamaha, badala yake alinikemea na kuniambia nirudi jela kwa kuwa mimi ni muuaji,"Alieleza Monicah.

Cha kusikitisha zaidi ni kuwa Monicah alipata wanawe wamefukuzwa na mwanamke huyo.

"Jambo ambalo liliniuma ni kuwa mwanamke huyo aliwafukuza watoto wangu wawili  wakiwa na umri wa chini na hakujali wataenda wapi, walielekea kwa ddada yangu ambaye aliwalea kama watoto wake, ningekuwa nataka kulipiza kisasi lakini Mungu alinionekania licha yamakovu yangu, sasa nashukuru Mungu kwa yale nilipitia kwani yamekuwa hadithi ya maisha yangu."

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved