logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fenerbahce wamuongeza Valencia kwenye picha ya mastaa Ronaldo na Messi

Kitendo hicho kilituma ujumbe kuwa Valencia ni staa wa tatu baada ya Ronaldo na Messi, kulinhana na Fenerbahce.

image
na Radio Jambo

Habari21 November 2022 - 08:39

Muhtasari


• Ronaldo na Messi kwa mara ya kwanza walionekana kweney picha ya pamoja nje ya uwanja, picha ambayo imezungumziwa sana duniani.

Messi na Ronaldo katika picha ambayo Valencia aliongewa kupitia photoshop

Jumapili mashindano ya kombe la duni yaling’oa nanga nchini Qatar ambapo wenyeji walifungua uwanja dhidi ya Ecuador majira ya saa moja jioni.

Katika mechi hiyo ambayo iliona rekodi ya miaka 92 kuvunjiliwa mbali, Ecuador walikiuka adabu za mgeni na kumchachafya mwenyeji mabao mawili kwa nunge mbele ya umati wa mashabiki wa nyumbani.

Mabao yote mawili yalifungwa na aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Manchester United ambaye sasa anaitumiakia Fenerbahce ya Uturuki, Enner Valencia.

Kufuatia kufungwa kwao mechi ya ufunguzi, Qatar iliingia kweney vitabu vya historia kuwahi kuwa taifa la kwanza kupoteza mechi ya ufunguzi nyumbani katika mashindano ya kombe la dunia, rekodi ambayo ilikuwa imedumu kwa miaka 92.

Valencia alifana katika mechi hiyo na aliibuka kuwa mchezaji bora na kutuzwa. Klabu yake ya Fenerbahce ilifurahia weledi wake na hawakusita kuihariri picha yake kando na picha ya masupastaa wawili wa soka Christiano Ronaldo na Lionel Messi – picha ambayo ilipakiwa katika mitandao ya kijamii ya mastaa hao Jumamosi usiku.

Wengi walisema kuwa picha hiyo ya Ronaldo na Messi ni moja ya picha ambazo zitaenda chini kama picha ya karene kwani haijawahi tokea waonekanai wakiwa pamoja nje ya uwanja wakipunga upepo kwa kufurahia mchezo wa chess.

Kitendo cha Fenerbahce kupakia picha hiyo ambayo walikuwa wameifanyia uhariri wa kiwango cha juu kwa kimombo Photoshop, walinuia kutuma ujumbe kuwa Valencia amejinafasi kando na wachezaji wawili mastaa wakubwa na kuwa yeye ndiye staa wa tatu baada ya kung’ara katika mechi ya ufunguzi wa kombe la dunia.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved