logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ofisi za UDA kaunti ya Siaya zateketezwa na waandamanaji

Ofisi hizo zinadaiwa kuchomwa na kundi la vijana wanaoshiriki katika maandamano.

image
na Davis Ojiambo

Habari30 March 2023 - 11:02

Muhtasari


  • • Uteketezaji huu unakuja wiki moja baada ya ofisi za UDA Kisumu kuchomwa.
Ofisi za UDA kaunti ya Siaya

Makao makuu ya chana cha UDA katika kaunti ya Siaya yametiwa moto na halaiki yenye ghadhabu ambao wameitikia wito wa maandamano ya Alhamisi kutoka kwa kinara wa upinzani Raila Odinga.

Katika picha na video ambazo zimeenezwa mitandaoni adhuhuri ya Alhamisi, ofisi hizo za chama tawala zinaonekana zikiteketea, am,bapo inaarifiwa kwamba ni kundi la vijana wanaoegemea mrengo wa Azimio waliotekeleza uteketezaji huo.

Aidha, haijabainika iwapo kuna uvamizi na wizi wa mali uliofanyika kabla ya kuteketezwa.

Haya yanakuja takribani wiki mbili baada ya ofisi zingine za UDA kaunti ya Kisumu kuporwa mali kabla ya kuharibiwa vibaya na kundi la vijana wanaoshiriki katika maandamano.

Katika uharibifu huo, pia gari moja lililokuwa nje ya ofisi hizo Kisumu liliteketezwa.

Uharibifu huo unafanyika wakati ambapo kinara wa Azimio na viongozi wengine wa muungano huo wakiwa katika msafara wa kuongoza maandamano jijini Nairobi, maeneo ya Imara Daima.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved