logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru alazimika kutoa walinzi wake kwa Mama Ngina baada ya walinzi wake kuondolewa

Uhuru Kenyatta sasa amelazimika kutoa baadhi ya walinzi wake ili kumlinda mamake.

image
na Davis Ojiambo

Habari24 July 2023 - 07:48

Muhtasari


    Rais mstaafu Uhuru Kenyatta sasa amelazimika kuwatuma baadhi ya walinzi wake kumlinda mamake na ambaye alikuwa mke wa Rais wa Kwanza,Mama Ngina Kenyatta.

    Maafisa hao wa polisi waliarifiwa na Uhuru kwenda kuwasaidia walinzi wa kibinafsi waliowekwa katika nyumba ya kibinafsi ya Mama Ngina katika mtaa wa Muthaiga, Nairobi, maafisa wanaofahamu suala hilo walisema.

    Haya yanajiri kufuatia uamuzi wa serikali kuwaondoa maafisa wa polisi wa utawala ambao wamekuwa wakilinda nyumba za mke huyo wa rais wa zamani Nairobi na Gatundu.

    Uhuru alisema maafisa hao ambao wamekuwa wakimlinda mamake kwa zaidi ya miaka 50 waliondolewa bila maelezo yoyote kwa familia hiyo.

    Mama Ngina hakuwepo wakati walinzi hao walipoondolewa mnamo Julai 18.

    Hapo ndipo Uhuru aliripotiwa kuwaambia baadhi askari waliokuwa wakilinda kwenda kulinda nyumba ya mamake kufuatia vitisho kwamba wahuni wangevamia.

    “Kama watanitaka waje kwa ajili yangu. Niko hapa. Hawapaswi kwenda kwa mama yangu mzee au watoto. Sitatishika. Niko tayari kutetea familia yangu,” alisema.

    Jumapili, Rais huyo msattafu alionekana katika uwanja wa Ngong Racecourse akifurahia mashindano ya farasi bila walinzi wowote.

    Uhuru alitengamana na wananchi waliokuwa wamehudhuria mashindano hayo kwa uhuru.


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved