logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke arekodiwa 'akimpiga' afisa wa kampuni ya maji kwa kumkatia maji - Video

Video hiyo imezua hisia tofauti, huku baadhi ya Waghana wakilaani tabia ya mwanamke huyo.

image
na Radio Jambo

Habari08 September 2023 - 09:26

Muhtasari


• Baadhi ya watu waliokuwa karibu wanaonekana wakijaribu kuingilia kati na kumsihi mwanamke huyo amwachie afisa huyo.

Mwanamke akimpiga mwanamume

Video moja imebuka mitandaoni ikimuonesha mwanamke mmoja alimdhalilisha wazi wazi mwanamume mmoja kwa kumkunja mashati huku watu wakishangilia.

Kwa mujibu wa blogu moja kutoka nchini Ghana, iliarifiwa kwamba mwanamume huyo aliyeonekana akikunjwa mashati ni mfanyikazi katika kamouni ya maji na alikuwa anadhalilishwa kwa madai kwamba alimkatia mwanamke huyo maji kwa kutolipa bili ya maji.

Video ya mwanamke huyo mwenye hasira akiwa amemshika afisa huyo kwenye eneo la shingo la shati lake la mikono mirefu, na kumburuta huku kukiwa na amri ya kumfungulia maji.

Afisa huyo asiyejiweza anaonekana kwenye video akihangaika bila matunda kujinasua kutoka kwa mshiko thabiti wa mwanamke huyo huku akiapa kutomuunganisha tena kwenye mfumo wa usambazaji maji.

Baadhi ya watu waliokuwa karibu wanaonekana wakijaribu kuingilia kati na kumsihi mwanamke huyo amwachie afisa huyo, lakini hakutaka kutetereka, badala yake, aliapa kutomtoa mikononi mwake hadi atakapomrudishia maji.

Video hiyo imezua hisia tofauti, huku baadhi ya Waghana wakilaani tabia ya mwanamke huyo na kutaka akamatwe na kufunguliwa mashitaka, huku wengine wakisema inawahudumia wafanyakazi wa GWC ipasavyo kwa sababu wanadaiwa kujulikana kwa kuwatendea vibaya wateja.

Tazama video hiyo hapa chini;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved