logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mafuriko Libya: Watu 5,300 wapoteza maisha huku kukiwa na wito wa msaada wa kibinadamu

Vyumba vya kuhifadhia maiti na hospitali zimezidiwa na miili.

image
na Davis Ojiambo

Habari14 September 2023 - 04:31

Muhtasari


  • • Kumekuwa na wito wa kutaka msaada zaidi wa kibinadamu huku waathiriwa wakiwa wamefunikwa na mifuko ya miili.

Zaidi ya watu 5,300 wanaaminika kufariki baada ya mafuriko katika mji wa Derna nchini Libya, afisa mmoja amesema.

"Bahari mara kwa mara inatupa maiti kadhaa," Hisham Chkiouat, waziri katika utawala wa mashariki mwa Libya alisema.

Kumekuwa na wito wa kutaka msaada zaidi wa kibinadamu huku waathiriwa wakiwa wamefunikwa na mifuko ya miili na wengine kuzikwa kwenye makaburi ya pamoja.

Mto wa maji ya mafuriko unaofanana na tsunami ulipiga Derna Jumapili baada ya bwawa kupasuka wakati wa kimbunga Daniel.

Vikosi vya uokoaji vinachimba vifusi vya majengo yaliyoporomoka kwa matumaini ya kupata manusura - lakini matumaini yanafifia na idadi ya waliofariki bado inatarajiwa kuongezeka zaidi.

Maafisa wanasema takribani watu 10,000 hawajulikani walipo, huku watu 30,000 wakikadiriwa kuwa wameyahama makazi yao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) nchini Libya lilisema Jumatano.

Vyumba vya kuhifadhia maiti na hospitali zimezidiwa na miili.

Daktari wa Libya Najib Tarhoni, ambaye amekuwa akifanya kazi katika hospitali karibu na Derna, alisema msaada zaidi unahitajika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved