logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mke wa meneja wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson amefariki dunia

"Familia inaomba faragha kwa wakati huu."

image

Habari06 October 2023 - 15:47

Muhtasari


  • Bendera katika uwanja wa Old Trafford zimeshushwa hadi nusu mlingoti na timu za kwanza za wanaume na wanawake zitavaa vitambaa vyeusi katika michezo yao mtawalia wikendi hii.

Lady Cathy Ferguson, mke wa meneja wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 84.

Familia ya Ferguson ilithibitisha habari hiyo katika taarifa iliyotolewa kwa shirika la habari la PA Ijumaa alasiri.

"Tuna masikitiko makubwa kuthibitisha kifo cha Lady Cathy Ferguson jana, aliyeacha mumewe, wanawe watatu, dada wawili, wajukuu 12 na kitukuu mmoja," ilisomeka taarifa hiyo.

"Familia inaomba faragha kwa wakati huu."

Bendera katika uwanja wa Old Trafford zimeshushwa hadi nusu mlingoti na timu za kwanza za wanaume na wanawake zitavaa vitambaa vyeusi katika michezo yao mtawalia wikendi hii.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved