logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mume aliyeshtakiwa kutelekeza wanawe adai shetani alimsukuma kumpa mkewe ujauzito

Yahaya alisema hakuwa na uwezo wa kumtunza binti yao mwenye umri wa miaka sita

image
na Davis Ojiambo

Habari31 October 2023 - 11:29

Muhtasari


  • • “Mimi ndiye baba wa mtoto. Sijaoana na mlalamikaji, ni kazi ya shetani kusababisha mimi kumpa ujauzito,” mlalamikiwa alisema.
Mahakama

Mfanyabiashara mmoja ambaye amefikishwa mahakamani na mpenzi wake kwa kushindwa kumtunza mtoto wake aliiambia mahakama kuwa hakuwa tayari kuzaa na kwamba shetani alimsukuma kumpa ujauzito mwanamke huyo.

Mwanamke huyo kwa jina Maryam Muhammad aliwasilisha ombi katika Mahakama huko Abuja kuamuru baba ya binti yake, Harisu Yahaya alipe matunzo ya mtoto huyo.

"Ninataka mahakama iamuru amtunze binti yake na kumlipia karo ya shule," Shirika la Habari la Nigeria (NAN) linamnukuu mlalamishi akisema katika ombi lake.

Alipofika mbele ya mahakama mnamo Jumatatu, Oktoba 30, 2023, Yahaya alisema hakuwa na uwezo wa kumtunza binti yao mwenye umri wa miaka sita, hasa shule ambayo ameandikishwa.

“Mimi ndiye baba wa mtoto. Sijaoana na mlalamikaji, ni kazi ya shetani kusababisha mimi kumpa ujauzito,” mlalamikiwa alisema.

Wakati Yahaya aliposema kuwa hana uwezo wa kulipia matunzo ya binti yake, Muhammad aliiambia mahakama kwamba hatajali kuondoa ombi la kutaka kumshurutisha kumtunza mtoto huyo ikiwa yuko tayari kumlea.

"Ana wazazi na binti yetu anaweza kukaa nao. Nitaondoa ombi langu la matunzo ikiwa atamchukua binti yetu," alisema.

Aliomboleza kwamba tangu kuzaliwa kwa msichana mdogo, Yahaya hajampa mahitaji yake, akimwachia mzigo peke yake.

Baada ya kusikia kutoka kwa mlalamikaji na mlalamikiwa, Ibrahim Rufai, hakimu alimwagiza Muhammad kuandaa ombi jipya la malezi na kumleta binti yake mahakamani siku inayofuata ya kusikilizwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved