logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jinsi Mfalme Charles alivyowafurahisha wengi kwa Kiswahili sanifu katika ikulu

Mfalme Charles yumo nchini kwa ziara ya siku nne.

image
na Davis Ojiambo

Habari01 November 2023 - 05:38

Muhtasari


  • • “Mabibi na mabwana, hamjambo? Niaje? Ni furaha yangu kubwa kuwa na nyinyi jioni ya leo…” mfalme Charles alisema kwa sehemu.
King Charles

Lugha ya Kiswaili ni moja ya lugha pendwa na zenye umaarufu Zaidi duniani.

Hili lilidhihirika Jumanne katika ikulu ya Nairobi wakati wa ziara ya mflame Charles wa tatu kutoka Uingereza.

Mfalme huyo akiandamana na mkewe Malkia Camilla na viongozi mbalimbali wa Kenya katika dhifa iliyoandaliwa katik ikulu ya Nairobi na mwenyeji wake Rais Ruto, aliwafurahisha wengi katika hotuba yake alipoamua kuzungumza Kiswahili.

Katika hotuba yake, mfalme alitaka kujichanganya na wasikilizaji wake; aliongea maneno machache ya Kiswahili japo kwa lafudhi yake kali ya kigeni, akiwaacha wasikilizaji katika vicheko. Katika hotuba yake, mfalme alistaajabu kupata fursa ya kurejea Kenya baada ya miaka mingi.

“Mabibi na mabwana, hamjambo? Niaje? Ni furaha yangu kubwa kuwa na nyinyi jioni ya leo…” mfalme Charles alisema kwa sehemu kabla ya kupigiwa makofi na kuendeleza hotuba yake kwa lugha yake ya nyumbani – Kiingereza.

Alitangulia kumsifu rais kwa mapokezi mazuri aliyopewa yeye na mkewe katika siku ya kwanza ya ziara yao ya kifalme barani Afrika. Mfalme huyo alijivunia kwa Kenya kuwa nchi yake ya kwanza kuzuru tangu kutawazwa kwake mwaka jana.

Pia alijutia madhira ambayo wapiganiaji uhuru wa Kenya walipitia mikononi mwa wakoloni wa taifa lake kati ya mwaka 1952 hadi 1960.

"Ni furaha kubwa kwa mke wangu na mimi kurejea Kenya kwa mara nyingine. Ninamshukuru sana rais kwa mwaliko wa ukarimu zaidi kwa ziara hii ya kiserikali; ukarimu mkubwa ambao mmetuonyesha na makaribisho mazuri ajabu,watu wa Kenya wametupokea. Imenigusa sana," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved