logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Naibu Rais Rigathi akutana na familia ya narehemu msanii Ally B

Rigathi  Gachagua  apeana pole,kwa familia ya Ally B,huku akiaidi kuwasaidia kimaisha

image
na Davis Ojiambo

Habari15 November 2023 - 11:53

Muhtasari


  • •Naibu wa Rais aliandamana  mwanasiasa na mwanamuziki Jaguar
Gachagua akutana na familia ya Ally B

Naibu wa Rais Rigathi Gachagua mapema leo ameshapisha taarifa  kwenye mtandao wake wa X akiwa  pamoja na  familia ya aliyekuwa msanii Ally B ambaye alifariki siku chache zilizopita.

Kulingana na naibu wa rais msanii huyo alikuwa maarufu kwa utunzi wa nyimbo huku akisema kuwa Ally B alichangia sana katika uchanguzi wa mwaka 2022 kwa ushawishi wake kwa vijana wa pwani.

 "Leo asubuhi katika Makazi Rasmi hapa Mombasa, niliikaribisha familia ya marehemu Mwanamuziki Ali Mwakaribu Ally B, aliyefariki mapema mwezi huu kwa ajili ya kuwafariji na kuwatia moyo,...

Ally B aliinuka kutoka katika hali ya unyonge alipiga hatua ya kitaifa kwa nyota yake ya muziki, ambao ulimfafanua kama mtu binafsi mwenye kipaji cha kipekee,Pia namkubuka kwa usaidizi wake usioyumba wakati wa kampeni zetu za uchaguzi,"ulisoma ujumbe wa Rigathi.

Naibu wa rais  Pia alichapisha  ujumbe maalum kutoka kwa Rais Ruto amboa alisema alitumwa na Rais.

"Natuma faraja yangu  tunapoendelea kuombea Roho ya Ally B ipumzike kwa Amani ya Milele, tutatembea maisha haya pamoja na familia yake changa,tasnia ya Sanaa ya Ubunifu ni msingi wa Utawala wangu  tunapotafuta kukuza vipaji vinavyowezekana, sio tu kwa burudani na kuelimisha,"ulisema ujumbe wa Rais.

Naibu wa Rais aliandamana  mwanasiasa na mwanamuziki Jaguar.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved