logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Takriban watu 4 wafariki,5 wajeruhiwa baada ya jengo kuporomoka Eastleigh

Mkuu wa polisi wa Nairobi Adamson Bungei alisema wafanyakazi wanne waliuawa papo hapo.

image

Habari02 December 2023 - 14:02

Muhtasari


  • Aliongeza hawakutarajia kupata watu zaidi kwenye vifusi kwa kuwa wafanyakazi waliokuwa zamu wamehesabiwa.

Takriban wafanyikazi wanne waliuawa wakati jengo lililokuwa likijengwa liliporomoka katika eneo la Eastleigh Nairobi.

Tukio hilo lilitokea kando ya Barabara ya Muratina Jumamosi alasiri huku wafanyikazi wakiwa na shughuli nyingi kwenye eneo la tukio polisi na mashahidi walisema.

Mkuu wa polisi wa Nairobi Adamson Bungei alisema wafanyakazi wanne waliuawa papo hapo.

Aliongeza wengine sita walijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini.

“Tumethibitisha vifo vya watu wanne na kuna majeruhi sita kufikia sasa. Tunachunguza mkasa huo,” alisema.

 

Aliongeza hawakutarajia kupata watu zaidi kwenye vifusi kwa kuwa wafanyakazi waliokuwa zamu wamehesabiwa.

Hata hivyo, kazi ya uokoaji na utafutaji iliendelea.

Hili ni tukio la hivi punde zaidi kutokea mjini humo.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved