logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume 'mrembo' aonesha picha zake baada ya kufaulu upasuaji wa kubadili jinsia (Picha)

Bobrisky alinukuu, "Nzuri na ya kustarehesha, huo ni mtindo wangu."

image
na Radio Jambo

Habari20 January 2024 - 11:55

Muhtasari


• Katika picha zilizotikisa hewani mtandaoni, Bobrisky akiwa amevalia mavazi meusi, alionekana akiwa amekaa vizuri kwenye kitanda chake, akionyesha sura yake mpya.

Bobriksy

Crossdresser na sosholaiti wa Nigeria, Idris Okuneye anayejulikana zaidi kama Bobrisky amewasha taa za mchana kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuibuka na picha mpya kuonesha jinsi amerembeka baada ya kufaulu katika upasuaji mwingine wa kuboresha urembo wake.

Bobrisky ambaye ni mwanamume aliyebadili jinsia yake kufuatia msururu wa upasuaji hivi majuzi alifanyiwa upasuaji wa kuongeza maziwa yake na kulainisha ngozi yake ya mwili.

Bobrisky, ambaye alikuwa amefanyiwa upasuaji wa kukuza tezi ya matiti (Augmentation mammoplasty), alitumia ukurasa wake wa Instagram alipokuwa akishiriki baadhi ya picha zinazoonyesha umbo lake jipya la mwili.

Katika picha zilizotikisa hewani mtandaoni, Bobrisky akiwa amevalia mavazi meusi, alionekana akiwa amekaa vizuri kwenye kitanda chake, akionyesha sura yake mpya.

Bobrisky alinukuu, "Nzuri na ya kustarehesha, huo ni mtindo wangu."

Tazama picha zake hapa chini:

Bobriksy
Bobrisky
Bobrisky

Wiki iliyopita tuliripoti kwamba mwanasosholaiti huyo aliyebadili jinsia alitoa ratecard yake ghali ikionyesha bei za baadhi ya huduma ambazo anapeana.

Katika orodha hiyo, Bobrisky alidai kwamba kwa mtu anayetaka kukutana naye kwa ajili ya salamu tu, ni sharti alipe kima cha shilingi laki tatu na ushee.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved