logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waziri wa zamani wa Zanzibar ahojiwa kuhusu uhaba wa pombe kisiwani humo

Simai Mohamed Said alifika mbele ya kamati ya maadili ya chama hicho siku ya Jumanne lakini hakufichua kwanini aliitwa.

image
na SAMUEL MAINA

Habari07 February 2024 - 12:36

Muhtasari


  • •Simai Mohamed Said alifika mbele ya kamati ya maadili ya chama hicho siku ya Jumanne lakini hakufichua kwanini aliitwa.

Chama tawala cha Tanzania (CCM) kimemuhoji aliyekuwa waziri wa utalii wa Zanzibar wiki kadhaa baada ya kujiuzulu kutokana na uhaba wa pombe visiwani humo.

Simai Mohamed Said alifika mbele ya kamati ya maadili ya chama hicho siku ya Jumanne lakini hakufichua kwanini aliitwa.

"Ni kawaida kutembelea afisi ya chama, na mimi si msemaji wa mikutano, unaweza kupata mwenyekiti au katibu mkuu wa kamati kusema jambo," Bw Said aliwaambia waandishi wa habari mara baada ya mkutano huo.

Alikuwa amejiuzulu kama waziri wa utalii wiki mbili zilizopita, akitaja "mazingira yasiyopendeza na ya kutatiza ya kazi".

Kujiuzulu kwake kumehusishwa na uhaba wa pombe unaovikabili visiwa hivyo vya Tanzania, jambo ambalo linatishia sekta ya utalii ya mojawapo ya maeneo yanayoongoza kwa utalii barani Afrika.

Bei za bia zimepanda kwa karibu 100% baada ya msururu wa usambazaji kutatizwa na mabadiliko ya ghafla ya waagizaji.

Kabla ya kujiuzulu, Bw Said aliituhumu hadharani Bodi ya Kudhibiti Vileo Zanzibar (ZLCB) kwa kusimamia vibaya idara ya vileo.

Lakini Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi alimshutumu Bw Said kwa kuwa na mgongano wa kimaslahi, alipokuwa waziri.

Ripoti zinahusisha jamaa mmoja wa Bw Said na kampuni moja ya kuagiza pombe ambayo leseni yake haikuongezwa ili kuendelea kuhudumu.

Upungufu huo wa pombe unakuja huku kukiwa na ongezeko la watalii wanaowasili katika visiwa vya Tanzania.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved