logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna Ushahidi! Jacque Maribe aondolewa mashtaka ya mauaji

<ul> <li>Maribe aliachiliwa huru na hakimu Grace Nzioka wa mahakama ya sheria Milimani Ijumaa juu ya ukosefu wa ushaidi.</li> </ul>

image
na Davis Ojiambo

Habari09 February 2024 - 11:42

Muhtasari


  • Maribe aliachiliwa huru na hakimu Grace Nzioka wa mahakama ya sheria Milimani Ijumaa juu ya ukosefu wa ushaidi.

Mwanahabari Jacque Maribe ameachiliwa huru kuhusiana na kesi ya mauaji ya  mfanyibiashara Monica Kimani.

Maribe aliachiliwa huru na hakimu Grace Nzioka wa mahakama ya Milimani Ijumaa kwa ukosefu wa ushaidi.

Alikuwa mtuhumiwa wa pili kwa kesi ya mauaji ya Monica ambayo imekuwa ikiendelea kwa zaidi ya miaka 5.

Kulingana na hakimu Justice Nzioka, mashtaka dhidi ya Jacque haikuwekwa ipasavyo. 

"Ni maoni yangu kwamba shtaka lililoletwa dhidi ya mshtakiwa wa pili halikuwa shtaka sahihi" hakimu Grace Nzioka alisema.

" Je, kuna kosa nililolifanya pale mshtakiwa wa pili alipotoa maelezo kwa afisa mpelelezi wa kituo cha polisi cha Langata ambayo yalibainika kuwa si kweli? Sisemi zaidi. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma inajua wajibu wao."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved