logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Charlene Ruto kutoa zawadi ya 100K na kushiriki lunch na mtu mmoja mwenye bahati

Mwisho wa kutuma kazi zako za kibunifu urakuwa Machi 11.

image
na Radio Jambo

Habari21 February 2024 - 05:40

Muhtasari


• Shindano hilo linatoa nafasi kwa vijana kuonyesha ustadi wao katika kubuni nembo nzuri na mshindi atapokezwa kitika cha shilingi laki moja.

Binti Ruto

Binti wa kwanza wa taifa, Charlene Ruto amezindua shindano la kibunifu ambapo anawataka vijana wenye ustadi katika kuunda nembo za kidijitali kujitokeza ili kushiriki katika shindano hilo.

Kupitia ukurasa wake wa X, Binti Ruto alisema kwamba shirika la Mtandao wa Vijana wa Kimataifa linatafuta nembo nzuri ambayo inahusiana na masuala ya vijana katika ubunifu.

Shindano hilo linatoa nafasi kwa vijana kuonyesha ustadi wao katika kubuni nembo nzuri na mshindi atapokezwa kitika cha shilingi laki moja pamoja pia na kushiriki chakula cha mchana kwenye meza moja na Charlene Ruto.

“Mtandao wa Vijana wa Kimataifa (TYPNI) unatafuta nembo bainifu inayojumuisha ari ya ujana na ubunifu. Shindano hili linatoa fursa kwa wabunifu wachanga kuonyesha vipaji vyao na kuchangia utambulisho mahiri wa TYPNI,” aliandika kwenye bango hilo kwenye mtandao wa X.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved