logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto alazimika kuendelea na hotuba gizani baada ya stima kupotea akiongea (video)

"Tupo...Oh, sawa," Ruto alisema huku akijaribu kipaza sauti.

image
na Radio Jambo

Habari22 February 2024 - 06:03

Muhtasari


• Katika video ambayo ilinaswa katika mkutano huo, Ruto alisikika akiongea kutoka gizani huku akiuliza nni kinaendelea, dakika chache kabla ya umeme kurudi tena.

Rais Ruto gizani

Jumatano wakati wa kilele cha mkutano wa wajumbe wa serikali huko Naivasha, rais Ruto alilazimika kuendelea na maongezi yake gizani baada umeme kupotea kwa takribani mara mbili huku rais akiendelea na hotuba.

Katika video ambayo ilinaswa katika mkutano huo, Ruto alisikika akiongea kutoka gizani huku akiuliza nni kinaendelea, dakika chache kabla ya umeme kurudi tena.

Ruto alikuwa akiwahutubia wajumbe wa Baraza lake la Mawaziri kuhusu ni kwa nini aliwafanya kuwa chaguo lake katika serikali wakati taa zilizimika kwa angalau sekunde tano. Mkuu wa nchi alijaribu kuzungumza kupitia kwa kipaza sauti kwa muda kabla ya taa kuwasha tena.

"Tupo...Oh, sawa," Ruto alisema huku akijaribu kipaza sauti.

Lakini kama hiyo haikuwa aibu tosha kutoka kwa kampuni ya umeme KPLC, rais tena alilazimika kumaliza hotuba yake gizani baada ya stima kupotea akikaribia kuhitimisha.

Itakumbukwa katika siku za hivi karibuni, KPLC imekuwa ikikumbwa na kuyumba kwa mitambo yake ya kuzalisha umeme na kulitumbukiza taifa katika giza kwa saa kadhaa.

Hatua hii imeona baadhi ya watu wakitoa wito kwa rais kumsimamisha kazi waziri wa Kawi Davis Chirchir kwa kile wanahisi ni kuzembea kazini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved