logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kobbie Mainoo azungumza baada ya kuichezea Uingereza mara ya kwanza ilipochapwa 0-1 na Brazil

Mainoo alifurahi kucheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa siku ya Jumamosi usiku wakati Uingereza iliposhindwa 0-1 na Brazil.

image
na Radio Jambo

Habari24 March 2024 - 09:16

Muhtasari


•Mainoo alifurahi kucheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa siku ya Jumamosi usiku wakati Uingereza iliposhindwa 0-1 na Brazil.

•Uingereza  ilishindwa 0-1 na Brazil katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa W embley mwendo wa saa nne usiku wa Jumamosi.

alichezea Uingereza mara ya kwanza Jumamosi, Machi 23, 2024.

 Mchezaji chipukizi wa Manchester United, Kobbie Mainoo alifurahi kucheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa siku ya Jumamosi usiku wakati Uingereza iliposhindwa 0-1 na Brazil.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 18 alitambulishwa uwanjani katika dakika ya 75 akichukua nafasi ya kiungo wa Chelsea Connor Galagher. Hata hivyo hakuweza kuisaidia timu yake kuepuka kipigo cha aibu kwenye Uwanja wa Wembly.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchuano huo wa kirafiki, Mainoo alisema ni hisia ya kipekee ambayo hatasahau kucheza mchezo wake wa kwanza kwa England.

"Ni hisia maalum nikianza kucheza kimataifa kwa mara ya kwanza Wembley na mbele ya familia yangu," Mainoo alisema.

Aliongeza, "Ni wakati ambao sitasahau kamwe.”

Uingereza  ilishindwa 0-1 na Brazil katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa W embley mwendo wa saa nne usiku wa Jumamosi.

Mshambulizi Endrick mwenye umri wa miaka 17 ambaye kwa sasa anachezea Palmeiras alifunga bao pekee katika mechi hiyo katika dakika ya 80 na kuipa timu yake ushindi.

Lilikuwa bao la kwanza la kimataifa kwa mchezaji huyo mwenye kipaji ambaye anatarajiwa kujiunga na Real Madrid msimu ujao.

Beki wa Manchester City Kyle Walker naye hata hakumaliza kucheza kipindi cha kwanza kwani aliumia katika dakika ya 20 na kulazimika kutolewa nje ya uwanja.

Akizungumzia jeraha hilo, kocha wa Uingereza Gareth Southgate alisema wanajipanga kumtathmini ili kubaini kama ni mbaya sana.

“Bado hatujui. Anahisi kitu lakini yeye si mchezaji ambaye anaumia mara kwa mara kwa hivyo hana uhakika kabisa ni nini. Kwa hivyo ni jambo ambalo tunapaswa kutathmini katika siku zijazo," Southgate alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved