logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mechi ya Udinese dhidi ya Roma ililazimika kusitishwa baada ya beki kuzirai uwanjani

Udinese walitweet kwa urahisi: "Tuko pamoja nawe, Ndicka."

image
na Radio Jambo

Habari15 April 2024 - 08:18

Muhtasari


• “Mchezaji huyo ana fahamu na amepelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi. Forza Evan, sote tuko pamoja nawe!”

• Udinese walitweet kwa urahisi: "Tuko pamoja nawe, Ndicka."

Evan Ndicka wakati wa pambano dhidi ya Udinese.

Pambano la Jumapili la Serie A kati ya Udinese na Roma lilisitishwa baada ya mchezaji wa kimataifa wa Ivory Coast Evan Ndicka kuzimia uwanjani.

Beki huyo wa Roma mwenye umri wa miaka 24 alitoka nje ya uwanja kwa machela kunako dakika 72 kwenye Uwanja wa Bluenergy.

Klabu yake baadaye ilithibitisha kuwa mchezaji huyo wa zamani wa Auxerre na Eintracht Frankfurt alikuwa na fahamu na alikuwa amepelekwa hospitali kuchunguzwa.

Taarifa kwenye akaunti ya X rasmi ya Roma - iliyokuwa akaunti ya Twitter - ilisomeka: "Kufuatia dharura ya matibabu ya uwanjani iliyomhusisha Evan Ndicka, mechi kati ya Udinese na Roma imesimamishwa.”

“Mchezaji huyo ana fahamu na amepelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi. Forza Evan, sote tuko pamoja nawe!”

Udinese walitweet kwa urahisi: "Tuko pamoja nawe, Ndicka."

Roberto Pereyra alikuwa ameipatia timu ya nyumbani bao la kuongoza kabla ya mapumziko, lakini Romelu Lukaku akafanya matokeo kuwa 1-1 zikiwa zimepita dakika 64.

Taarifa hiyo iliongeza: "Ataendelea kuwa chini ya uangalizi kwa ajili ya vipimo hospitalini."

Ndicka alijiunga na Roma kwa uhamisho wa bure kutoka Eintracht Frankfurt mwaka 2023 na amecheza mechi 19 katika klabu hiyo ya Italia.

Mechi iliyosalia sasa imepangwa kuchezwa baadaye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved