logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Gachagua akutana na makanika wa Kariakor kujadili changamoto katika maeneo yao ya kazi

Bw Gachagua alidokeza kuwa serikali ya UDA inalenga kuboresha sekta zote za kazi.

image
na Radio Jambo

Habari24 April 2024 - 17:49

Muhtasari


•Makanika walikuwa wamelalamikia kuhusu kufurushwa na mazingira duni ya kazi, masuala ambayo waliwasilisha mbele ya naibu wa rais.

•"Tunabakia mstari wa mbele katika kuboresha mazingira ya kazi kwa kila sekta ili kustawi kwa sababu kila harakati ni muhimu," Gachagua alisema.

akishiriki mazungumzo na mwanahabari Muthoni Wakirumba wakati wa mkutano na makanika wa Nairobi nyumbani kwake Karen mnamo Aprili 24, 2024.

Siku ya Jumatano, naibu rais Rigathi Gachagua alikuwa na mkutano wa kushirikisha na wawakilishi wa makanika kutoka mItaa ya Kariokor na Grogon jijini Nairobi kufuatia malalamishi ambayo walikuwa wameibua.

Mafundi hao walikuwa wametumia vyombo vya habari kuangazia baadhi ya changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo wakifanya kazi jijini. Walikuwa wamelalamikia kuhusu kufurushwa kutoka maeneo yao ya kazi na mazingira duni ya kazi, masuala ambayo waliwasilisha mbele ya naibu wa rais nyumbani kwake Karen, Nairobi.

Akizungumza kwenye taarifa baada ya mkutano huo, Bw Gachagua alibainisha kuwa serikali ya UDA inalenga kuboresha sekta zote za kazi.

“Utawala wa Ruto unatanguliza usikilizaji na mazungumzo ili kuelewa na kufahamu suluhu za vitendo kwa changamoto za wananchi, hasa zile zilizo katika sehemu ya chini kabisa ya piramidi ya kijamii na kiuchumi. Kufuatia wasiwasi ulioibuliwa na mafundi wa mitambo kutoka Kariokor kupitia vyombo vya habari kuhusu kufukuzwa na mazingira ya kazi yasiyo na heshima, leo, katika Makao Rasmi ya Karen, nilikaribisha wawakilishi wao kwa maongezi ya kuelewa changamoto zao,” Gachagua alisema kwenye taarifa aliyoichapisha kwenye mtandao wake wa kijamii. akaunti.

Aliongeza, "Tunabakia mstari wa mbele katika kuboresha mazingira ya kazi kwa kila sekta ili kustawi kwa sababu kila harakati ni muhimu."

alishikii mkutano na makanika wa Nairobi nyumbani kwake Karen mnamo Aprili 24, 2024.

Katika mkutano huo, naibu rais alibainisha kuwa kila kazi ni muhimu na kusisitiza kuhusu dhamira ya serikali katika kuboresha mazingira ya kazi katika sekta zote.

Mwanahabari wa Kikuyu Muthoni Wakirumba ambaye pia alikuwepo katika mkutano huo alimshukuru kiongozi huyo kwa kuwapa sikio mafundi hao na kueleza imani kuwa sasa watapata mazingira bora ya kufanyia kazi.

“Kuna Mungu mbinguni. Makanika kutoka Kariakor na Grogon hatimaye watapata nafasi nzuri ya kazi. H.E Rigathi Gachagua, Mungu akubariki,” alisema kupitia Facebook

Gachagua pia alisisitiza  kwamba mchango wa kila mtu katika uchumi ni muhimu sana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved