logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jaguar amtaka Eric Omondi kufanya kazi na serikali kusaidia wananchi

Ninashukuru kile Eric Omondi anajaribu kufanya, lakini haitaleta matokeo yoyote

image
na

Habari03 May 2024 - 11:27

Muhtasari


•"Maafa ni makubwa kuliko Eric Omondi," Jaguar alisema

•Ninashukuru kile Eric Omondi anajaribu kufanya, lakini haitaleta matokeo yoyote

Mwanamuziki mkongwe aliyegeuka kuwa mwanasiasa Charles Njagua Kanyi almaarufu Jaguar anamtaka aliyekuwa mcheshi Eric Omondi kufikiria kufanya kazi na serikali.

Jaguar, ambaye  alikuwa Mbunge wa Starehe kwa miaka 5, alibainisha kuwa kazi anayofanya Eric Omondi ni ya kupongezwa lakini inaweza kuwa bora zaidi ikiwa ataungana na serikali badala ya kutupia serikali lawama.

"Maafa ni makubwa kuliko Eric Omondi," Jaguar alisema.

Aliendelea kubainisha kuwa chochote alichokuwa anafanya mchekeshaji huyo ni kikubwa lakini ana shaka kuwa mtu mmoja anaweza kuleta mabadiliko makubwa.

Katika video inayovuma hivi sasa kwenye Instagram mwanamuziki huyo wa zamani alisisitiza kwamba ikiwa Eric angeungana na serikali basi mabadiliko anayotarajia kuleta yanaweza kupatikana kwa urahisi na bora zaidi.

 

“Nashukuru kwa lolote analofanya lakini sidhani litaleta mabadiliko, binafsi ukiniuliza ni kubwa kuliko yeye naona ni vyema akashirikiana na serikali na kufanya nao kazi ili kuleta mabadiliko," Jaguar alisema waziwazi wakati wa mahojiano aliyokuwa nayo na WanaYouTube.

Jaguar aliendelea kutaja baadhi ya mambo ambayo Eric alifanya hasa wakati huu ambapo taifa limekumbwa na mvua kubwa na mafuriko akiangazia kuwa baba wa watoto 2 hangeweza kuokoa kila mtu hata akitaka.

“Mfano ukiangalia Athi River alikoenda kusaidia watu Kenya nzima inaathirika, ni vizuri ata kama anapiga serikali ashikane na serikali kama anataka kusaidia.

Ninashukuru anachojaribu kufanya, lakini haitaleta mabadiliko yoyote. Haitaleta athari kubwa kwa sababu ni kubwa kuliko chochote anachofikiria,"  Jaquar ilisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved