logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sehemu ya barabara ya UN kuelekea Runda yafungwa na KURA kutokana na mafuriko

Mamlaka imewataka madereva kutumia njia mbadala za kuelekea wanakoenda.

image
na

Habari06 May 2024 - 07:05

Muhtasari


•Kura imetangaza kufunga sehemu ya barabara ya Umoja wa Mataifa ya Runda kutokana na mafuriko.

•Mamlaka iliwataka madereva kutumia njia mbadala kuelekea wanakoenda.

Mamlaka ya Barabara za Mijini nchini (Kura) imetangaza kufunga sehemu ya barabara ya Umoja wa Mataifa ya Runda kutokana na mafuriko.

Katika taarifa yake Jumatatu, Mamlaka hiyo ilisema barabara hiyo imefungwa kutokana na kuendelea kuongezeka kwa kina cha maji katika barabara hiyo.

Ilisema haya ni matokeo ya mvua kubwa iliyonyesha Jumapili usiku.

“Mamlaka ya Barabara za Mijini ya Kenya inasikitika kufahamisha umma kwamba UN-Avenue, Runda imefungwa kutokana na maji kupanda barabarani kufuatia mvua kubwa iliyonyesha jana usiku.

"Sehemu zilizoathiriwa ni kati ya mzunguko wa Barabara ya Ruaka na Magnolia karibu. (Mkahawa wa Lord Erroll)." sehemu ya taarifa hio ilisema.

Mamlaka imewataka madereva kutumia njia mbadala za kuelekea wanakoenda.

Kura aliongeza kuwa wataendelea kufuatilia hali ilivyo.

"Tunafuatilia kwa karibu hali ilivyo na tutatoa taarifa kuhusu maendeleo. Tunawaomba madereva kutumia njia mbadala na kuchukua tahadhari."

Mvua kubwa inayoendelea kunyesha jijini Nairobi na kote nchini imesababisha uharibifu mkubwa wa mali pamoja na kupoteza maisha.

Hii pia imeshuhudia kufungwa kwa barabara, miongoni mwa hatua zingine zinazochukuliwa na serikali kuwaweka Wakenya salama.

Watu wamehimizwa kuhamia maeneo ya juu na salama kutokana na mafuriko nyumbani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved