logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bangi yapatikana katika magunia manne ya maharage Moyale

Bangi yafichwa katika magunia manne ya maharage yaliyokamatwa Moyale

image
na Radio Jambo

Habari07 May 2024 - 06:57

Muhtasari


•Maafisa hao wanasemekana kutumia mbwa wa kunusa ambaye alitambua kitu cha kutiliwa shaka ndani ya magunia hayo.

• Misokoto 22 ya bangi yenye thamani ya Kshs.435,000  ilipatikana ndani ya gunia hizo.

Maafisa wa upelelezi katika Kaunti Ndogo ya Moyale walinasa dawa za kulevya zilizohifadhiwa kwenye magunia manne ya maharagwe Jumatatu kufuatia taarifa kutoka kwa umma.

Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ilisema kwamba maafisa walipokea ripoti za "mtu anayeshukiwa na magunia manne ya maharagwe" katika kituo cha mabasi ya Liban na kusababisha jibu la haraka la polisi.

"Walipofika, waligundua kuwa magunia hayo yalikuwa yameachwa bila mtu yeyote kwenye lango la afisi hiyo  ya kukata tiketi, na mwenye nyumba hakupatikana, kwani alidaiwa kuwa alienda kutafuta karatasi za kuidhinishwa na ofisi ya KRA," DCI ilisema kwenye X.

Maafisa hao wanasemekana kutumia mbwa wa kunusa ambaye alitambua kitu cha kutiliwa shaka ndani ya magunia hayo.

Maafisa kisha walipeleka magunia hayo hadi afisi za DCI Moyale ambako yalifunguliwa, na kufichua misokoto 22 ya bangi yenye thamani ya Kshs.435,000.

Shehena hio inawekwa chini ya ulinzi hili kutumika kama ushahidi.

Wakati huo huo, msako mkali unaendelea kuwatafuta washukiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved