logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kifo cha balozi wa Urusi, Msumbiji yachunguza

Rais Filipe Nyusi alisema kifo cha Surikov kiliacha "pengokubwa".

image
na Radio Jambo

Habari15 May 2024 - 04:33

Muhtasari


• Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma wa Msumbiji imesema kuwa haikufahamu madai ya kukataa kwa mamlaka ya Urusi kufanya uchunguzi wa mwili.

Serikali ya Msumbiji imesema inashirikiana na mamlaka mjini Moscow kuchunguzakifo cha Balozi wa Urusi Alexander Surikov.

Surikov, 68, alipatikana amekufa Jumamosi usiku katika makazi yake rasmi katika mji mkuu wa Msumbiji, Maputo, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Chanzo cha kifo chake bado hakijajulikana.

Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma wa Msumbiji imesema kuwa haikufahamu madai ya kukataa kwa mamlaka ya Urusi kufanya uchunguzi wa mwili wa balozi huyo kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari vya ndani.

Katika taarifa, Rais Filipe Nyusi alisema kifo cha Surikov kiliacha "pengokubwa", akimtaja kama mwanadiplomasia aliyejitolea na sifa za kipekee, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Surikov aliteuliwa katika nafasi hiyo mnamo 2017.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved