logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchungaji Kanyari ataka msamaha kutoka kwa Prince Mwiti

leo nilikuwa nimekasirika sana, Mungu akanijia, nikakuona umepiga magoti mbele yangu

image
na

Habari15 May 2024 - 08:15

Muhtasari


•Mwiti  alisema kuwa Kanyari ni mlaghai na akamuonya mhubiri huyo  asithubutu kumuibia nyota yake mwiti.

•Price Mwiti na Mchungaji Kanyari walizozana kwenye TikTok moja kwa moja baada ya Mwiti kushutumu maisha ya mchungaji huyo.

MCHUNGAJI VICTOR KANYARI

Mhubiri mwenye utata Mchungaji Victor Kanyari alitaka msamaha kutoka kwa Prince Mwiti baada ya kumtusi kwenye mtandao wa TikTiok.

Mwiti alichukua  mtandao wake waTikTok kumvua nguo mhubiri huyo kwa maneno yake akimtaja Kanyari kuwa mwizi.

“Uliibia watu pesa, ukaibia watu nyota halafu ukaja kujifanya nabii wa uongo, wewe ni mmoja wa manabii wa uongo hapa, tayari Bwana amejiweka mbali nawe, unanilaani, unamhutubia nani hapa TikTok. ?

Natumai kuwa  kile unaanza unaweza kukimaliza. Je, ni kwa sababu ilikuwa vigumu kwako kuiba nyota yangu? ."

Kanyari alizungumzia suala hilo kupitia mtandao wake wa TikTok, akisema kwamba alikasirishwa na TikToker huyo.

“Leo nahutubia Mwiti, leo nilikuwa nimekasirika sana, Mungu akanijia, nikakuona umepiga magoti mbele yangu, Nikaona ukiniomba ukisema nabii usinitumie kinyunyu, nilikuwa nikutumie kitu ukiwa umelala na lini unaamka ungeuliza umepatwa na nini, Mungu aliniambia nisitoe panga nililotaka kuua lakini Mungu aliniomba nikusamehe.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved