logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kate Actress:Baadhi yetu hatuhitaji kulipiwa nauli kwenda US

Mwigizaji Kate amewakosoa wanaofikiria kuwa safari yake ya Marekani ilifadhiliwa na pesa za walipa kodi

image
na Radio Jambo

Habari23 May 2024 - 11:27

Muhtasari


•Mwigizaji Kate amefichua kuwa alijifadhili mwenyewe kwenye safari yake ya Marekani

Catherine Kamau

Mwigizaji wa Kenya Catherine Kamau almaarufu Kate Actress amewajibu wakosoaji wanaodai safari yake ya kwenda Marekani inafadhiliwa na pesa za walipa kodi.

 Mwigizaji huyo alimjibu  shabiki mmoja aliyekomenti kwenye picha  yake instagram. '...baadhi yetu hatuhitaji fedha za serikali ili kustawi,safari hii inajifadhili kikamilifu, hii ni mimi kuwekeza kwenye brand yangu na kuzingatia biashara yangu ..Unapaswa kujaribu," alisema Kate .

Kwenye Instagram, Mwigizaji  Kate alisema kwamba safari hiyo inalenga kukuza brandi yake na amejifadhili mwenyewe.Alifafanua kuwa mwaliko wake ulikuwa kwa hisani ya ubalozi wa Marekani.

 Siku zilizopita,mwigizaji huyo aliyeshinda tuzo za mwigizaji bora;alitumia akaunti yake rasmi ya mtandao wa kijamii kufichua mwaliko wake wa kuhudhuria chakula cha jioni cha Jimbo katika Ikulu ya White House na Luncheon kwenye studio maarufu ya Tyler Perry huko Atlanta.

Taarifa hio ilisoma;

”Habari za asubuhi, msichana huyu wa kijijini atahudhuria mlo wa jioni wa Serikali katika Ikulu ya White House na Chakula cha mchana katika Studio za Tyler Perry huko Atlanta kwa mwaliko kutoka kwa Mheshimiwa Balozi Meg Whitman.

Eddie Butita pia yuko Marekani baada ya kuandamana na Rais William Ruto katika ziara yake ya kiserikali ya siku tatu nchini Marekani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved