logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama maeneo yatakayoathirika na kukatizwa kwa umeme leo, Jumapili- KPLC

Kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

image
na Radio Jambo

Habari26 May 2024 - 05:58

Muhtasari


•Kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

•Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Uasin Gishu, Kisii, Mombasa na Kilifi.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumapili, Mei 26.

Katika taarifa ya Jumamosi jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti tano za Kenya yatakosa umeme kati ya saa moja asubuhi na saa kumi na moja jioni.Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Uasin Gishu, Kisii, Mombasa na Kilifi.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu kadhaa za mtaa wa Westlands zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja.

Kituo cha Sinendet katika kaunti ya Uasin Gishu kitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa nne asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za mji wa Kisii katika kaunti ya Kisii zitakosa umeme kati ya saa moja na dakika ishirini asubuhi na saa kumi na dakika ishirini alasiri.

Sehemu kadhaa za maeneo ya Ganjoni na Kizingo katika kaunti ya Mombasa zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Wakati huohuo, baadhi ya sehemu za maeneo ya Mtwapa na Kanamai katika kaunti ya Kilifi pia zitashuhudia kukatizwa kwa umeme.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved