logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke akamatwa kwa kumpiga mawe mume hadi kifo kwa mzozo wa Ksh.3,000 Makueni

Syombua Musau anadaiwa kumpiga mumewe kwa mawe mgongoni na kumuua papo hapo.

image

Habari27 May 2024 - 13:02

Muhtasari


  • Kulingana na Albanus Mutula, msaidizi wa chifu wa eneo hilo, wanandoa hao walitofautiana kuhusu Ksh.3,000 huku marehemu akimshutumu mkewe mchanga kwa kuiba pesa hizo.

Polisi Mbooni Mashariki, Kaunti ya Makueni wanamshikilia mwanamke mwenye umri wa miaka 32 nayedaiwa kumuua mumewe mwenye umri wa miaka 82.

Kulingana na Albanus Mutula, msaidizi wa chifu wa eneo hilo, wanandoa hao walitofautiana kuhusu Ksh.3,000 huku marehemu akimshutumu mkewe mchanga kwa kuiba pesa hizo.

Syombua Musau anadaiwa kumpiga mumewe kwa mawe mgongoni na kumuua papo hapo.

Mwanamke huyo anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Mbumbuni akisubiri kusomewa mashitaka.

Mwili wa mzee huyo ulipelekwa katika chumba cha maiti cha Tawa.

Msimamizi huyo aliwataka wakazi kutafuta njia mwafaka za kutatua tofauti zao bila kuchukua hatua za kurudi nyuma.

uy67

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved