logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume afariki dunia kwenye injini ya ndege Amsterdam

Polisi wa kijeshi wa Netherland pia walisema kuwa wameanza uchunguzi.

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2024 - 09:55

Muhtasari


  • Kifo hicho kilitokea wakati ndege ya KL1341 ilipokuwa ikijiandaa kuondoka kuelekea Billund, Denmark, Jumatano alasiri.

Mtu mmoja afariki dunia baada ya kuishia kwenye injini ya ndege ya abiria ya KLM katika uwanja wa ndege wa Schiphol mjini Amsterdam.

Kifo hicho kilitokea wakati ndege ya KL1341 ilipokuwa ikijiandaa kuondoka kuelekea Billund, Denmark, Jumatano alasiri.

Shirika hilo la ndege limesema linawahudumia abiria na wafanyakazi walioshuhudia tukio hilo na linaendelea na uchunguzi.

Polisi wa kijeshi wa Netherland pia walisema kuwa wameanza uchunguzi.

Kikosi cha Royal Netherlands Marechaussee kiliongeza katika ujumbe kwenye mtandao wa X kwamba abiria na wafanyikazi wote wameondolewa kwenye ndege.

Marehemu bado hajatambuliwa na ni mapema mno kusema ikiwa ilikuwa ajali au aina ya kujitoa uhai, msemaji aliliambia shirika la habari la Reuters.

Vyombo mbalimbali vya habari vya Uholanzi vimependekeza mwathiriwa anaweza kuwa mfanyakazi anayehusika katika kuelekeza ndege kurudi nyuma kabla ya kupaa.

Picha zilizopatikana na shirika la utangazaji la taifa la Uholanzi NOS zinaonyesha huduma za dharura zinazozunguka ndege ya abiria kwenye uwanja wa ndege - ambapo ndege huegeshwa.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved