logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama maeneo yatakayoathirika na kukatizwa kwa umeme leo, Alhamisi- KPLC

Kaunti ambazo zitaathirika ni Nairobi, , Nyeri, Tharaka Nithi Kiambu na Mombasa.

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2024 - 05:02

Muhtasari


•Kampuni ya KPLC ilisema kukatizwa kwa umeme kunatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

•Kaunti ambazo zitaathirika ni Nairobi, , Nyeri, Tharaka Nithi Kiambu na Mombasa.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Mei 30.

Katika taarifa ya Jumatano jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kunatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

Kampuni ilisema baadhi ya maeneo ya kaunti tano za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na  moja jioni.Kaunti ambazo zitaathirika ni Nairobi, , Nyeri, Tharaka Nithi Kiambu na Mombasa.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu kadhaa za mtaa wa Utawala zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Wamagana na Mbaaini katika kaunti ya Nyeri zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi alasiri.

Sehemu kadhaa za maeneo ya Kiraro na Kianjagi  katika kaunti ya Tharaka Nithi pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa nane mchana.

Katika kaunti ya Kiambu, sehemu kadhaa za maeneo ya Ndula, Kolping, Nyacaba, Maraba, Ondiri, Karai, Riabai, na Migaa zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Wakati huohuo, baadhi ya sehemu za maeneo ya Miritini, Bonje, na Mazeras katika kaunti ya Mombasa pia zitaathirika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved