logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wezi wamvamia afisa mkuu wa polisi akiwa amelala na kumpiga, kumuibia pesa na runinga

Afisa huyo aliyevamiwa kwa sasa anaripotiwa kuwa katika hali nzuri akipokea matibabu hospitalini.

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2024 - 13:33

Muhtasari


• Jarida hilo linaripoti kwamba tayari vijana 4 wamekamatwa kutokana na tukio hilo lililojiri Jumanne.

Mwanamke mjamzito apatikana amedungwa visu mgongoni

Vitengo vya polisi nchini Uganda vimeanzisha uchunguzi kubaini wahusika katika tukio ambalo afisa mkuu wa polisi alivamiwa na genge la watu waliokuwa wamejihami nyakati za usiku akiwa amelala kabla ya kumshambulia na kumuibia mfuko wa pesa na runinga na kutokomea gizani.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor, mkuu huyo wa polisi kitengo cha Superitendent alivamiwa na kundi hilo la vijana wenye silaha nyumbani kwake majira ya saa tisa alfajiri akiwa amelala na kumpiga vibaya kabla ya kutoroka na mfuko wa hela na runinga.

Jarida hilo linaripoti kwamba tayari vijana 4 wamekamatwa kutokana na tukio hilo lililojiri Jumanne.

“Wahuni hao walipata njia ya kuingia nyumbani kwa afisa wa polisi wakati akiwa amelala. Waliiba runinga ya kisasa yenye thamani ya shilingi milioni 1.2 [Za Uganda], mfuko wa begi uliokuwa na kiasi cha hela kisichokadirika kwa sasa kabla ya kumtia majeraha mabaya. Wezi hao baadae walitoroka kutoka kwa eneo la tukio,” jarida hilo lilimnukuu polisi anayesimamia uchunguzi huo.

Kwa sasa, washukiwa wanne wanaodaiwa kuhusika na shambulizi hilo wamekamatwa na mamlaka, huku juhudi zikiendelea za kurejesha mali iliyoibwa.

"Kwa msaada wa kitengo cha mbwa, wapelelezi wetu waliweza kuwasaka washukiwa. Bado hawajafichua walikoweka vitu vilivyoibiwa. Hilo sasa ndilo lengo letu," aliongeza.

Afisa huyo aliyevamiwa kwa sasa anaripotiwa kuwa katika hali nzuri akipokea matibabu hospitalini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved