logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC yatangaza maeneo ambako stima zitapotea leo Jumatatu

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Bomet, Nandi, na Kisii.

image
na Radio Jambo

Habari03 June 2024 - 04:30

Muhtasari


•KPLC imetangaza kuwa baadhi ya maeneo ya kaunti tatu za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi alasiri. 

•Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Bomet, Nandi, na Kisii.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatatu, Juni 3.

Katika taarifa ya siku ya Jumapili jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti tatu za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi alasiri. 

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Bomet, Nandi, na Kisii.

Katika kaunti ya Bomet, baadhi ya sehemu za maeneo ya Silibwet, Merigi na Tenwek zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi alasiri.

Sehemu kadhaa za maeneo ya Chebarbar, Baraton University, na Kipchapo Factory katika kaunti ya Nandi zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.

Katika kaunti ya Kisii, baadhi ya sehemu za maeneo ya Geteri, na Kanyimbo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tano asubuhi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved