logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mlipuko wa lori la gesi Embakasi waibua maswali mengi

Naam, wananchi wameagizwa kuchukua hatua mwafaka hasa mikasa kama hii inapotokea.

image
na

Habari03 June 2024 - 12:20

Muhtasari


  • Watu wawil wameaga dunia baada ya gari lililokuwa likisafirisha gesi aina ya LPG kulipuka.
  • Visa vya mlipuko wa malori ya gesi vimekuwa vikishuhudiwa huku kisa cha leo kikiwa cha hivi punde
  • Ni wajibu wa serikali zote mbili kujishirikisha katika kutathmini usawa wa makampuni 
Moto Embakasi

Watu wawil wameaga dunia baada ya gari lililokuwa likisafirisha gesi aina ya LPG kulipuka.

“so apparently ni gari ilikuwa imebeba magari then kuna yenye ilikuwa inaleak ndani so huyo mubaba mwenye alikuwa anaendesha akaenda kunusa sijui hakusikia ama ni LPG hatukufika huko karibu. Akaenda kuwasha gari, kueka ignition ndio hiyo, ikalipuka.” Ndiyo iliyokuwa sauti ya shahidi.

Msongamano mkubwa wa magari umeshuhudiwa katika eneo la Outering road karibu na Fedha Avenue 1 kwenye eneo bunge la Embakasi Magharibi.

Aidha mlipuko huo umewawacha wengi wakiwa wamebung’aa kwani visa hivi vya mlipuko wa malori ya gesi vimekuwa vikishuhudiwa huku kisa cha leo kikiwa cha hivi punde.

“Tunaomba serikali kuu na serikali ya kaunti ziingilie kati katika kufanya uchunguzi wa kina kuhusu visa hivi vya milipuko ya gesi kwani ni suala linaloanza kuwa la mazoea sana."

"Vilevile, ni wajibu wa serikali zote mbili kujishirikisha katika kutathmini usawa wa makampuni haya iwapo yana vibali vinavyostahili na kustahiki katika uendeshaji wa operesheni zao ili kusiweze tokea mikasa mingine zaidi ya milipuko ya gesi,” alisema Victor Kulundu.

Naam, wananchi wameagizwa kuchukua hatua mwafaka hasa mikasa kama hii inapotokea. Vilevile, hali hii imezidi kuibua hisia mbalimbali huku wengi wakihofia hali yao ya usalama.

“Si kawaida kwa sababu mikasa hii inazidi kutokea moja baada ya nyingine. Hii si kawaida hasa katika eneo la Embakasi. Serikali ifanye uchunguzi wa kina na upelelezi zaidi ili tujue niaje milipuko hii inazidi kutokea moja baada ya nyingine kama misururu,” alisema Chris Ambutsi.

Mpaka sasa haijang’amuliwa ni watu wangapi wamejeruhiwa na shughuli za uokozi bado zinaendelea kufanyika katika eneo hilo la mkasa huu.   


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved