logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbosso akiri kupata mtoto na aliyekuwa mke wa kakake Alikiba

Ndiyo, nina mtoto na yule mwanamke ambaye awali aliolewa na Abdu Kiba.

image
na

Habari04 June 2024 - 11:40

Muhtasari


•Ninajaribu kadiri niwezavyo kuwa na uhusiano mzuri naye lakini wakati mwingine ni ngumu, tuko hapa na tunashughulika na mtoto.

•Ni swala ambalo lilileta maswala mengi sana kwenye mahusiano yetu maana nilikuwa muwazi sana kwake lakini alikuwa hajaniambia mambo mengi

Mwimbaji wa Tanzania Mbosso amekiri kupata mtoto na mwanamke ambaye aliwahi kuolewa na mdogo wa Alikiba, Abdukiba.

Muimbaji huyo wa WCB alifunguka hayo alipokuwa akihojiwa na Wasafi FM hivi karibuni ambapo alikiri kuhusika na mwanadada huyo hadi kufikia hatua ya kuwa na mtoto naye.

"Ndiyo, nina mtoto na yule mwanamke ambaye awali aliolewa na Abdu Kiba," Mbosso alisema.

Kulingana na Mbosso, hakuwahi kufahamu uhusika wowote kati ya mama yake mzazi na ndugu huyo wa Ali Kiba.

Mwimbaji huyo aliendelea kumlaumu mwanadada huyo akisema aliiweka ndoa yake na Abdukiba kuwa siri kwa muda mrefu hivi kwamba yeye (Mbosso) alikuja kujifunza mengi baadaye.

"Ni swala ambalo lilileta maswala mengi sana kwenye mahusiano yetu maana nilikuwa muwazi sana kwake lakini alikuwa hajaniambia mambo mengi. Nilipokuja kugundua kuwa ni mke wa zamani wa Abdu Kiba, nilikuwa nimechelewa." Alieleza.

Ingawa anajilaumu kwa kutochukua muda kumjua mpenzi wake wa wakati huo, Mbosso anasema kilichobaki ni wao kumlea mtoto waliyemzaa pamoja.

"Ninajaribu kadiri niwezavyo kuwa na uhusiano mzuri naye lakini wakati mwingine ni ngumu, tuko hapa na tunashughulika na mtoto.

Kadhalika, Mbosso alikiri kuwa na uhusiano mbaya na mwanadada huyo akisema hawakuzungumza lakini wanagombana karibu kila mara wanapozungumza.

"Tunazungumza lakini tunagombana sana. Kuna wakati tunatupiana cheche za maneno na hatuwezi kumaliza mwezi bila kugombana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved