logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Biashara zangu huniingizia pesa zaidi ya muziki wangu-Diamond

Mwimbaji huyo alisema alikuwa akipata pesa zaidi kutoka kwa biashara zake zingine.

image
na Radio Jambo

Habari06 June 2024 - 09:19

Muhtasari


  • Mbali na kuwa mwanamuziki, mwimbaji huyo anamiliki lebo ya muziki ambayo imewasajili Zuchu, Mbosso, Lava Lava, DVoice na Queen Darleen.

Staa wa bongo kutoka Tanzania Diamond Platnumz anasema kama angekuwa anaangalia kiasi cha pesa anachoingiza kwenye tasnia ya muziki basi angeachana na muziki huo.

Mwimbaji huyo alisema alikuwa akipata pesa zaidi kutoka kwa biashara zake zingine.

"Ili ukue, lazima uwe na majukumu zaidi ambayo yataongeza pesa zaidi. La sivyo, ningetoka kwenye tasnia ya muziki," alisema.

Akiongeza, "Biashara nilizo nazo sasa zinaniingizia pesa zaidi kuliko muziki ninaofanya."

Aliendelea kushauri "Lakini hutakiwi kuondoka, unahitaji tu kuongeza kazi zaidi."

Mbali na kuwa mwanamuziki, mwimbaji huyo anamiliki lebo ya muziki ambayo imewasajili Zuchu, Mbosso, Lava Lava, DVoice na Queen Darleen.

Hapo awali, lebo hiyo iliwasajili Harmonize, Rayvanny, na Rich Mavoko kabla ya kuondoka.

Diamond pia anamiliki media house ambayo ina TV na kituo cha redio. Mwimbaji huyo pia ni balozi wa chapa kadhaa ikiwa ni pamoja na chapa ya pombe, chapa ya simu na chapa ya mawasiliano.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved