logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzia! 7 waaga dunia katika ajali ya barabarani Meru

Polisi waliripoti kuwa wengine kadhaa walijeruhiwa na kulazwa hospitalini.

image

Habari23 June 2024 - 08:40

Muhtasari


  • Kulingana na mamlaka, lori hilo lilikuwa likisafirisha vitalu vya ujenzi kutoka Meru kuelekea Timau wakati dereva alishindwa kulidhibiti mwendo wa saa kumi na mbili na dakika 20 usiku.

Takriban watu saba waliuawa Jumamosi jioni baada ya lori moja kuacha barabara na kugonga pikipiki na watembea kwa miguu katika eneo la Timau kaunti ya Meru.

Polisi waliripoti kuwa wengine kadhaa walijeruhiwa na kulazwa hospitalini.

Kulingana na mamlaka, lori hilo lilikuwa likisafirisha vitalu vya ujenzi kutoka Meru kuelekea Timau wakati dereva alishindwa kulidhibiti mwendo wa saa kumi na mbili na dakika 20 usiku.

Waliofariki ni pamoja na wanaume wanne, wanawake wawili na msichana mmoja, miongoni mwao mpanda pikipiki ambaye alitangazwa kufariki alipofika katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Timau.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Buuri Laura Imbacha alisema kuwa watu kadhaa waliojeruhiwa walipelekwa katika vituo vya matibabu katika miji ya Timau na Nanyuki.

"Lori hilo liliigonga pikipiki, ambayo iliondolewa kutoka eneo la tukio hadi eneo lisilojulikana. Baadaye iliwaangusha watembea kwa miguu kadhaa, ikabingiria mara kadhaa na kutua kwenye shimo," polisi walisema.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved