logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waandamanaji waharibu na kupora klabu ya Timba XO inayohusishwa na Oscar Sudi

Klabu hiyo ilifunguliwa rasmi wiki chache zilizopita wakati wa hafla iliyohudhuriwa na Oscar Sudi.

image
na Davis Ojiambo

Habari25 June 2024 - 13:11

Muhtasari


  • •Klabu hiyo ilifunguliwa rasmi wiki chache wakati wa hafla iliyohudhuriwa na Sudi na wabunge wengine kadhaa.

Waandamanaji mjini Eldoret walivamia, kuharibu na kupora klabu moja mjini Eldoret inayohusishwa na mbunge wa kapseret Oscar Sudi.

Klabu hiyo inayojulikana kama Timber XO iko kando ya barabara ya Eldoret kuelekea Nairobi. Klabu hiyo ilifunguliwa rasmi wiki chache zilizopita wakati wa hafla iliyohudhuriwa na Sudi na wabunge wengine kadhaa

Waandamanaji hao waliandamana kutoka Eldoret CBD hadi kwenye klabu ambapo walivamia na kuharibu kuta za vioo, madirisha na milango.

Polisi walifika huku baadhi ya waandamanaji wakiingia kwenye klabu na kuondoka na baadhi ya vitu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved