Afisa wa magereza mwanamke nchini Uingereza ameshtakiwa kufuatia kupatikana kwa video ya mtandao wa kijamii inayodaiwa kumuonyesha akifanya mapenzi na mfungwa katika gereza la HMP Wandsworth, kusini magharibi mwa London, ripoti ilisema.
Linda De Sousa Abreu, 30, kutoka Fulham, magharibi mwa London, anakabiliwa na mashtaka ya utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma. Anatarajiwa kufika katika Mahakama.
Polisi wa Metropolitan walianzisha uchunguzi siku ya Ijumaa baada ya video hiyo, inayodaiwa kurekodiwa ndani ya gereza hilo, kusambaa mtandaoni.
Kanda hiyo inaripotiwa kuonyesha afisa huyo mwanzoni akiwa amevalia sare kamili kabla ya kujihusisha na kitendo hicho.
HMP Wandsworth, gereza la enzi ya Victoria lililojengwa mnamo 1851, limekuwa likikabiliana na msongamano mkubwa wa watu na hali mbaya, The Guardian walieleza.
Ukaguzi wa hivi majuzi ulifunua masuala yanayosumbua, ikiwa ni pamoja na vurugu zilizokithiri, wanyama waharibifu, na changamoto kali za wafanyikazi.
Kituo hicho, kilichoundwa kwa ajili ya wafungwa wachache zaidi, kwa sasa kinafanya kazi kwa asilimia 163 ya uwezo wake uliokusudiwa, na kinahifadhi zaidi ya wafungwa 1,500.
Msemaji wa Scotland Yard alithibitisha uchunguzi unaoendelea. "Rushwa ya wafanyikazi haivumiliwi, na afisa wa zamani wa gereza anayedaiwa kuonyeshwa kwenye video hii ameripotiwa kwa polisi," mwakilishi wa Jeshi la Magereza alisema.