logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PCS Mudavadi na DP Gachagua waponea shoka la kutupwa nje Ruto akivunja baraza la mawaziri

Kando na mawaziri wote kwenda nyumbani mara moja, pia mwanasheria mkuu wa serikali, Justine Muturi alipatwa na shoka hilo.

image
na Davis Ojiambo

Habari11 July 2024 - 13:05

Muhtasari


  • • Hata hivyo, waziri mwenye mamlaka makuu Musalia Mudavadi na naibu rais Rigathi Gachagua waliponea shoka hilo kwani nyadhifa zao hazikuathirika na mageuzi hayo ya rais Ruto.
MUDAVADI NA GACHAGUA

Rais William Ruto Alhamisi alasiri alifanya mageuzi makubwa katika baraza lake la mawaziri baada ya kulivunjilia mbali na kuwatuma mawaziri wote nyumbani.

Rais katika hotuba yake kwa taifa, alitangaza kwamba baada ya kutathmini kwa muda mrefu, alilazimika kufanya maamuzi hao magumu ya kuwafukuza mawaziri wote kisha kuanza safari mpya ya matumaini katika serikali yake.

Kando na mawaziri wote kwenda nyumbani mara moja, pia mwanasheria mkuu wa serikali, Justine Muturi alipatwa na shoka hilo.

Hata hivyo, waziri mwenye mamlaka makuu Musalia Mudavadi na naibu rais Rigathi Gachagua waliponea shoka hilo kwani nyadhifa zao hazikuathirika na mageuzi hayo ya rais Ruto.

“Nimeamua kuwafuta kazi mara moja Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Baraza la Mawaziri la Kenya isipokuwa Waziri mwenye mamlaka makuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Masuala ya Diaspora na bila shaka Ofisi ya Naibu Rais haiathiriwi kwa njia yoyote," alisema.

Ruto alisema kuwa atashiriki katika mashauriano ya kina katika sekta mbalimbali na mirengo ya kisiasa na Wakenya wengine kwa jumla.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved