logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto kuhutubia taifa kwa mara nyingine leo saa nane alasiri

Kulingana na Katibu wa Habari wa Ikulu Emmanuel Talam, Rais atahutubia nchi kutoka Ikulu ya Nairobi.

image
na SAMUEL MAINA

Habari11 July 2024 - 09:10

Muhtasari


  • •Kulingana na Katibu wa Habari wa Ikulu Emmanuel Talam, Rais atahutubia nchi kutoka Ikulu ya Nairobi.

Rais William Ruto anatarajiwa kuhutubia taifa saa nane mchana.

Kulingana na Katibu wa Habari wa Ikulu Emmanuel Talam, Rais atahutubia nchi kutoka Ikulu ya Nairobi.

Agenda ya kikao cha rais na waandishi wa habari, hata hivyo, bado haijulikani.

Ruto mnamo Ijumaa alidokeza kutekelezwa kwa baadhi ya mabadiliko katika serikali hivi karibuni.

Alitoa dokezo hilo wakati wa hotuba kwa taifa ambapo alitangaza hatua kadhaa za kubana matumizi ili kuokoa gharama serikalini.

Hotuba ya Alhamisi inajiri siku tatu tu baada ya Ruto na kiongozi wa Upinzani Raila Odinga kuitisha mazungumzo ya kitaifa kuanzia Jumatatu, Julai 15.

Mazungumzo hayo yatakuwa na angalau washiriki 150, kati yao 50 wakiwakilisha vijana.

Baada ya wito huo, baadhi ya wanasiasa wa Upinzani walisema hawatakuwa sehemu ya kikao hicho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved