logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Martin Khafafa achukua nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Radio Africa Group

Tangazo hilo lilitolewa na mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Radio Africa Group Kiprono Kittony siku ya Jumatano.

image
na SAMUEL MAINA

Habari24 July 2024 - 10:28

Muhtasari


  • •Tangazo hilo lilitolewa na mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Radio Africa Group Kiprono Kittony siku ya Jumatano.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Radio Africa Martin Khafafa.

Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Radio Africa Group Martin Khafafa amechukua nafasi ya Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni.

Tangazo hilo lilitolewa na mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Radio Africa Group Kiprono Kittony siku ya Jumatano.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji Patrick Quarcoo kustaafu kutoka Radio Africa Group baada ya kuitumikia kwa miaka 24.

Katika tangazo hilo, Kittony alisema hakuna mabadiliko makubwa katika kampuni hiyo.

"Martin Khafafa sasa ndiye Mkurugenzi Mtendaji mpya kuanzia leo na hakuna mabadiliko mengine mapya katika usimamizi," Kittony alisema.

Kittony alipitisha mawasiliano hayo wakati wa tafrija ya kumuaga Mkurugenzi Mtendaji wa zamani Quarcoo ambaye alistaafu kuanzia Julai 24, 2024.

Kittony aliwaomba wafanyakazi wa Radio Africa kumuunga mkono Khafafa anapochukua nafasi hiyo mpya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved