logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wale wameondoka upinzani kwenda serikalini kwaherini, mimi nabaki na watu - Babu Owino

Owino alisisitiza kwamba yeye atasalia na wananchi huku akiahidi kutoa taarifa rasmi baadae Alhamisi.

image
na Davis Ojiambo

Habari25 July 2024 - 06:03

Muhtasari


  • • Tamko hili lilijiri saa chache baada ya rais Ruto kutangaza kundi la pili la baraza lake la mawaziri. 
  •  
    • Katika hotuba yake kwa nchi adhuhuri ya Jumatano, rais Ruto aliwajumuisha wanachana 4 wa ODM katika baraza lake la nawaziri.
BABU OWINO

Mbunge wa Embakasi Mashariki Paul Ongili maarufu kama Babu Owino amevunja kimya chake baada ya sehemu ya wanachama wa ODM kuingia katika serikali ya Rais Ruto.

Kupitia kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii, Owino aliwatakia kila la kheri wale wameamua kuondoka katika mrengo wa upinzani wa Azimio na kujiunga katika serikali ya Kenya Kwanza.

Owino alisisitiza kwamba yeye atasalia na wananchi huku akiahidi kutoa taarifa rasmi baadae Alhamisi.

"Nabaki imara kusimama na Wananchi wa Kenya. Waliotoka upinzani na kujiunga na Serikali,KWAHERINI. Nitatoa taarifa yangu rasmi kesho.Aluta continua," Owino alisema.

Tamko hili lilijiri saa chache baada ya rais Ruto kutangaza kundi la pili la baraza lake la mawaziri. 

Katika hotuba yake kwa nchi adhuhuri ya Jumatano, rais Ruto aliwajumuisha wanachana 4 wa ODM katika baraza lake la nawaziri.

Wanne hao ni manaibu wa chama cha ODM Hassan Joho na Wycliffe Oparanya, mwenyekiti wa kitaifa John Mbadi na kiongozi wa wachache katika bunge la kitaifa Opiyo Wandayi. 

Joho atakuwa anaongoza wizara ya madini na uchumi wa baharini, Oparanya atakuwa waziri wa vyama vya ushirika na SMEs, Wandayi atakuwa waziri wa nishati huku Mbadi akichukua wizara ya Fedha.

Uamuzi huu ulionekana kujiri kutokana na mashauriano ya kinara wa ODM Raila Odinga na rais William Ruto wiki chache zilizopita.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved