Kikao cha kusikiliza utetezi wa naibu wa rais Rigathi Gachagua kimeairishwa hadi saa kumi na moja jioni ambapo Gachagua anatarajiwa kufika mbele ya seneti kujitetea.
Hili limetukia baada ya wakili anayewakilisha naibu huyo wa rais Paul Muite, kuambia seneti kuwa mteja wake ni mgonjwa na amelazwa katika hospitali moja jijini Nairobi.
Naibu wa rais Rigathi Gachagua amekosa kufika mbele ya seneti kujitetea dhidi ya madai kumi na moja yaliyowasilishwa dhidi yake na bunge la kitaifa kwa bunge la seneti huku wakili wake Paul Muite akiambia seneti kuwa mteja wake ameugua..
Wakili wa Gachagua amemwomba spika Kingi kumruhusu muda wa saa mbili ili kumwona mteja wake pamoja na daktari hospitalini.
Spika Kingi kufuatia hayo amemkubalia muda huo ila amesema kwamba ikiwa naibu wa rais Rigathi
Gachagua hatafika bungeni humo kwa wakati uliowekwa, maseneta wataendelea na
vikao hivyo.
Kulingana na spika, suala
ambalo liko mbele ya seneti linazingatia sana muda uliowekwa kukamilika