Aliyekuwa Mkuu wa magereza Wycliffe Ogalo na Mkuu wa Gereza la Kamiti Charles Mutembei watiwa mbaroni

Muhtasari
  • Aliyekuwa Mkuu wa magereza Wycliffe Ogalo na Mkuu wa Gereza la Kamiti Charles Mutembei watiwa mbaroni
Aliyekuwa Mkuu wa magereza Wycliffe Ogalo atiwa mbaroni
Image: Laura Shatuma

Kamishna Mkuu wa Magereza ya Kenya Wycliffe Ogalo na Mkuu wa Gereza la Kamiti Charles Mutembei wamekamatwa na maafisa wa upelelezi wa DCI. 

Kukamatwa kwa wawili hao kunakuja muda mfupi baada ya Rais Uhuru Kenyatta kubatilisha uteuzi wa Ogalo kama Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Kenya.

Nafasi yake ilichukuliwa na Brigedia mstaafu John Warioba ambaye aliapishwa mara moja.

Mabadiliko hayo yanafuatia kutoroka kwa hivi majuzi kwa wafungwa watatu wa ugaidi katika gereza la Kamiti Maximum.

"Mheshimiwa Rais leo amemteua na kushuhudia kuapishwa kwa Brigedia (Mst) John Kibaso Warioba kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza," taarifa kutoka Ikulu ilisema.

Waliotoroka ni pamoja na Mohamed Ali Abikar, ambaye alihukumiwa kwa jukumu lake katika shambulio la Chuo Kikuu cha Garissa 2015 ambapo watu 148 waliuawa.

Mtu wa pili alikamatwa mwaka wa 2012 kutokana na shambulio lililozuiwa dhidi ya bunge la Kenya na wa tatu kwa kujaribu kujiunga na kundi la wanamgambo wa al-Shabab nchini Somalia.

The former Commissioner-General of Prisons Wycliffe Ogalo was arrested moments after President Uhuru Kenyatta announced his sacking. https://bit.ly/3ovPsdi Subscribe for more videos: https://bit.ly/2mPyDy3 Connect with The Star Online Online on: WHATSAPP: https://bit.ly/2p8IC2e TELEGRAM : https://bit.ly/2oszlSe Sign Up To THE STAR WEBSITE for Exclusive content: FACEBOOK: https://bit.ly/2ot4G7m TWITTER: https://bit.ly/2mPoH7K INSTAGRAM: https://bit.ly/2mPoZLS Email NEWSLETTER: Visit The Star WEBSITE: https://www.the-star.co.ke/