logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna ushahidi! Jacque Maribe aondolewa mashtaka ya mauaji ya Monica Kimani

Mwanahabari Jacque Maribe ameachiliwa huru katika kesi ya mauaji ya Monica Kimani.

image
na SAMUEL MAINA

Habari09 February 2024 - 09:52

Muhtasari


  • •Mwanahabari Jacque Maribe ameondolewa mashtaka katika kesi ya mauaji ya mfanyibiashara Monica Kimani.
akiwa katika Mahakama ya Milimani, mbele ya Hakimu Grace Nzioka mnamo Februari 9, 2024, wakati wa hukumu ya kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani .

Mwanahabari Jacque Maribe ameachiliwa huru katika kesi ya mauaji ya Monica Kimani.

Maribe aliachiliwa na Jaji Grace Nzioka wa Mahakama ya Milimani mnamo Ijumaa, kwa kukosa ushahidi.

Yeye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo ambayo imekuwa ikiendelea kwa zaidi ya miaka mitano.

Kulingana na Jaji Nzioka, shtaka lililotolewa dhidi ya Maribe halikuwekwa ipasavyo.

"Ni maoni yangu kwamba shtaka lililoletwa dhidi ya mshtakiwa wa pili halikuwa shtaka sahihi," alisema.

"Je, kulikuwa na kosa lolote wakati mshtakiwa wa pili alipotoa taarifa kwa afisa wa upelelezi katika kituo cha polisi cha Lang'ata ambayo ilibainika kuwa si kweli? Sisemi tena. Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma inajua wajibu wao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved