logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Sitakuangusha kwa upendeleo ambao umenipa” – DP Kindiki amwambia rais Ruto

"Hivyo nakuahidi mbele ya huu umati na mbele ya Mungu kwamba sitakuangusha kwa upendeleo ambao umenipa leo,” Kindiki aliongeza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Hivi Punde01 November 2024 - 11:20

Muhtasari


  • "Hivyo nakuahidi mbele ya huu umati na mbele ya Mungu kwamba sitakuangusha kwa upendeleo ambao umenipa leo,” Kindiki aliongeza.
  • Kindiki alifika katika ukumbi wa kuapishwa, Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Kenyatta (KICC) 

Naibu wa rais mpya Profesa Kithure Kindiki ametoa ahadi ya kipekee kwa rais William Ruto, pindi baada ya kula kiapo kuhudumia taifa chini yake kama naibu wa rais.

Akizungumza kaitka ukumbi wa KICC katika hafla ya kipekee ya kuapishwa kwake, Kindiki alimshukuru Ruto na kumtaja kama mwalimu wake wa kisiasa na kuahidi kwamba hatokuja kumuangusha hata siku moja katika majukumu yake atakayompa.

“Mheshimiwa rais, maneno yamenikosa kujieleza jinsi ninavyo na furaha leo. Niseme kwamba ninamshukuru Mwenyezi Mungu ambaye anaongoza kila hatua na kila kitu cha kila mwanadamu duniani. Nina shukurani kwako rais kwa heshima ambayo umenipa kufanya kazi chini yako,” Kindiki alisema.

“Mheshimiwa rais, mimi nimekuwa mwanafunzi wako wa kisiasa kwa karibia miaka 20 sasa, na hakuna kitu katika ulingo wa kisiasa ambacho kimenisaidia kujifunza zaidi ya muda ambao nimetembea na kufanya kazi karibu na wewe katika nafasi tofauti. Kwa hivyo mheshimiwa rais ninashukuru. Hivyo nakuahidi mbele ya huu umati na mbele ya Mungu kwamba sitakuangusha kwa upendeleo ambao umenipa leo,” Kindiki aliongeza.

Anamrithi aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambaye alitimuliwa. Kabla ya kuteuliwa na Rais William Ruto, Kindiki aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa.

Baadaye alithibitishwa na Bunge. Kiti cha majaji watatu katika Mahakama ya Juu kiliondoa amri zilizokuwa zimezuia kiapo cha Kindiki siku ya Alhamisi.

Kindiki alifika katika ukumbi wa kuapishwa, Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Kenyatta (KICC) 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved