Corona

Donald Trump Jr apatikana na virusi vya corona

Watu wengi klatika Familia ya Trump wamepata maambukizi hayo na kupona

Muhtasari
  •  Don Junior amekosolewa kwa kupuuza athari za Corona 
  • Babake na mamake wa kambo Melania ni miongoni mwa walioambukziwa hapo awali 

 

Donald Trump Jr

 

 Mwanawe wa kiume wa  rais wa Marekani  Donald Trump  amepatikana na virusi  vya corona kulingana na msemaji .

 Donald Trump Jr,  mwenye umri wa miaka 42  alipatikana na ugobnjwa huo mwanzoni mwa wiki hii  na amekuwa akijitenga katika karantini  tangu matokeo hayo yalipotolewa .

" Hajakuwa na daalili zozote  na anafuata kanuni zote za matibabu kuhusu covid 19’ imesema taarifa iliyotolewa

Don Jr   ni mtoto wa pili wa Trump kupatikana na virusi hivyo bada ya Barron Trump mwenye umri wa miaka 14 kupatikana na ugonjwa huo mwezi uliopita lakini sasa amepona .

 Don Junior alikuwa nguzo muhimu sana katika kampeini za babake  na kumekuwa na uvumi kwamba naye pia angependa kugombea urais siku zijazo .

 Mpenzi wake Don Jr  ,Kimberly Guilfoyle,  aliyekuwa akitangaza katika kituo cha Fox  alipatikana na virusi hivyo mwezi Julai  na pia akapona .Hakupata ugonjwa huo wakati huo .

 Mapema siku ya ijumaa  msaidizi maalum wa rais  Andrew Giuliani,  alitangaza pia kwamba amepatikana na virusi vya corona .

Mr Giuliani,  ni mtoto wa wakili wa rais Trump Rudy Giuliani,  alisema katika twitter kwamba alikuwa akishuhudia ishara chache za kuugua  baada ya kupokea matokeo yake siku ya ijumaa asubuhi .

Mapema mwezi huu  mkuu wa wafanyikazi katika White House Mark Meadows  alikuwa miongoni mwa maafisa wakuu waliopatikana na virusi vya Corona .  Rais Trump mwenyewe alilazwa hospitalini kwa siku tatu mwanzoni mwa mwezi oktoba baada ya kupatikana na virusi hivo .Mkewe Melania Trump pia aliambukizwa na akapona