Wanamgambo 21 wa Al-Shabab wauliwa kwa risasi baada ya mahakama ya Somalia kuwapata na hatia

Redio ya serikali ilisema kuwa 18 kati yao walikuwa wametekeleza mauaji na ulipuaji wa mabomu kwa zaidi ya muongo mmoja.

Muhtasari

•Wanaume ishirini na moja wameuawa katika jimbo lenye uhuru wa Somalia la Puntland baada ya kupatikana na hatia ya kuwa wanachama wa kundi la wanamgambo wa  al-Shabab.

•Walihukumiwa na mahakama ya kijeshi huko Galkayo na kupigwa risasi na kikosi maalum kilichojihami kwa bunduki .

Wanamgambo wa Al shabaab ambao walipigwa risasi
Wanamgambo wa Al shabaab ambao walipigwa risasi
Image: Hisani

Wanaume ishirini na moja wameuawa katika jimbo lenye uhuru wa Somalia la Puntland baada ya kupatikana na hatia ya kuwa wanachama wa kundi la wanamgambo wa  al-Shabab.

Walihukumiwa na mahakama ya kijeshi huko Galkayo na kupigwa risasi na kikosi maalum kilichojihami kwa bunduki .

Wanamgambo 18 wa Al-sabaab wakisubiri kupigwa risasi
Wanamgambo 18 wa Al-sabaab wakisubiri kupigwa risasi
Image: Hisani

Redio ya serikali ilisema kuwa 18 kati yao walikuwa wametekeleza mauaji na ulipuaji wa mabomu kwa zaidi ya muongo mmoja.

Hukumu kama hizo za kifo zilikuwa zimetolewa na mahakama katika maeneo mengine ya Somalia hapo awali.

Lakini hii inaripotiwa kuwa idadi kubwa zaidi ya mauaji ya wafuasi wa al-Shabab kuwahi kutokea Puntland.

Mamlaka huko Puntland zilikuwa zimeapa kuwafikisha mahakamani wafuasi wa al-Shabab au watu watakaopatikana wakisaidia kundi hilo katika mashambulio yake.

(Maongezi: Samuel Maina)